Mikwara ya Simba si mchezo, Stand watimuana

MIKWARA ya Simba ambayo jana Jumatano jioni ilitua hapa Shinyanga, imeitia mchecheto Stand United na kupiga chini baadhi ya vigogo wake pamoja na kuwaweka pembeni kwa muda wengine.
Simba ambayo imerudi kwenye kasi yake katika Ligi Kuu Bara, itacheza na Stand Jumapili mjini hapa, katika mechi ya awali jijini Dar es Salaam Simba ilitoka sare ya bao 1-1 na timu hiyo ngeni kwenye Ligi Kuu.
Mashabiki wa Simba wameanza kumiminika mjini hapa huku viongozi wa juu wakionekana hapa na pale kuweka maandalizi sawa ingawa mashabiki wa Stand ambayo wamechanganyika na wale wa Yanga wameonekana kujidhatiti vilivyo.
Tayari Stand imewasimamisha kazi viongozi wa ufundi ambao ni Mkurugenzi wake, Muhibu Kanu, Kocha Msaidizi Emmanuel Masawe na wachezaji wake watatu Iddi Mobi, Khamisi Shengo na Mussa Kimbu.
Katibu Msaidizi wa klabu hiyo, Kennedy Nyange alisema uamuzi huo umefanyika wikiendi iliyopita kwenye kikao chao cha ndani.
Barua aliyoandika na Katibu wa Stand United, Soclaf Mkavilavya ilieleza kuwa Kanu alisimamishwa kwa sababu ameshindwa kutekeleza majukumu yake na kusababisha usumbufu kwa viongozi.
Pia barua hiyo ilimtaka akabidhi nyaraka zote za klabu na asiendelee kujishughulisha na shughuli yoyote ya kiutendaji na atalipwa nusu mshahara kila mwezi hadi hapo uamuzi mwingine utakapofikiwa, kama hataridhishwa ana haki ya kukata rufaa. Kanu alisema hatambui kusimamishwa wala tuhuma zake.
Mbali na mechi ya Simba Jumapili, mechi nyingine siku hiyo ni Azam na Tanzania Prisons pamoja na Yanga na Mbeya City.
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment