PROFESA TIBAIJUKA: SINA SABABU YA KUJIUZULU

Waziri Tibaijuka akizungumza na wanahabari.
Waandishi wa habari wakiwa kwenye mkutano…

UMATI wa waandishi wa habari ulifurika leo katika Ukumbi wa Hotel Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam ili kusikiliza ni nini atazungumza Waziri wa Nyumba na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka ambaye ni mmoja wa watuhumiwa wa sakata la uchotwaji wa fedha za akaunti ya Tegeta Escrow.
Akizungumza na wanahabari, Profesa Anna alisema: “Sioni sababu ya kujiuzulu kwa sababu mimi sio mtumishi wa wizara hiyo (Nishati na Madini), nilichopokea mimi ni msaada wala sijaona kitu kibaya zaidi ya kufurahia msaada huo ambao unasaidia shule ya watoto kike kama ninavyoomba na kupewa na watu wadau wengine kama Reginald Mengi.

Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment