YANGA ROHO JUU YAPEWA SIKU 90

MASTAA wanane wa Yanga ambao wengi wao wanacheza katika kikosi cha kwanza, wamebakiza miezi mitatu tu katika mikataba yao ya sasa na watakuwa huru mwishoni mwa msimu, Mwanaspoti imebaini.
Hata hivyo, uongozi wa klabu hiyo licha ya kutotaja majina ya mastaa hao, umesisitiza kwamba watapambana kiume kuhakikisha hakuna yeyote atakayechoropoka klabuni hapo.
Katibu wa Yanga, Jonas Tiboroha alikiri mastaa hao wanaelekea ukingoni mwa mikataba yao na kudai klabu hiyo ilifanya makosa kuchelewa kuwaandalia mikataba mipya, lakini ametoa ahadi nzuri kwa wapenzi wa klabu hiyo kuwa hakuna mchezaji muhimu atakayeondoka mwishoni mwa msimu kama ilivyotokea msimu uliopita.
“Ni kweli tuna wachezaji kama wanane ambao mikataba yao imebakiza miezi michache, itamalizika mwishoni mwa msimu, kuna makosa kidogo yalifanyika kukubali mikataba ya wachezaji wengi kufikia ukingoni kwa pamoja,” alisema Tiboroha ambaye ni msomi wa ngazi ya PHD.
“Kuna wachezaji ambao ni muhimu sana na mikataba yao nayo inakwisha, lakini hawataweza kuondoka kama ilivyokuwa kwa kina Frank Domayo na Didier Kavumbagu, tumeanza kazi ya kuangalia wale tunaowahitaji ili tuwapatie mikataba mipya.”
Katibu huyo ambaye ni mkufunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) aligoma kuweka wazi majina ya mastaa hao.
“Siwezi kusema ni nani na nani ambao mikataba yao inakwisha, itakuwa rahisi kwa wapinzani wetu kuwapata, kikubwa ni kwamba wote tunaowahitaji tutawaongezea mikataba na pia tutaanza mazungumzo na wale waliobakisha mwaka mmoja ili kuwaongeza, hatutaki tena wachezaji wengi wacheze wakiwa na mikataba ya miezi michache,” alisema Tiboroha.
“Katika hilo wanachana na mashabiki wetu waondoe wasiwasi kila kitu kitawekwa sawa.”
Hata hivyo, Mwanaspoti linafahamu kuwa miongoni mwa wachezaji hao ni kipa Deo Munishi ‘Dida’, beki Mbuyu Twite, Kiungo Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan na mshambuliaji Mrisho Ngassa.
Tayari mkataba wa Dida upo umeshaandaliwa lakini bado haujasainiwa na mazungumzo bado yanaendelea kwa Haruna na Twite ambao wanahitaji kubadilishiwa masilahi na dau la usajili ingawa habari za ndani zinadai kwamba wachezaji hao wanataka kupewa dau lote kwa mujibu wa makubaliano.
AIZUNGUMZIA
MECHI YA BDF
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment