Tunda Man Dubai kushoot video ya ‘Achana na Mimi’

Tunda Man anatarajia kwenda Muscat, Oman au Dubai kwenda kushoot video ya wimbo wake ‘Achana na Mimi.’
928930_1593523094211845_1730925003_n
Akizungumza na Bongo5 hivi karibuni, Tunda alisema ameamua kwenda Dubai kutokana na aina ya mazingira ambayo video yake inayahitaji.
“Nimepokea maoni ya video ya Achana na mimi kwahiyo nawa-promise kwamba nitafanya kwasababu nataka nikafanye Muscat au Dubai kwahiyo nilikuwa naangalia process za kwenda kule zinakuwaje,” amesema muimbaji huyo.
“Ndo mchakato ambao ninao sasa hivi nataka niushughulikie sasa hivi ili ikiwezekana mpaka mwezi wa tatu kazi iwe imeshatoka. Nimeamua kwenda kufanya Dubai kwa sababu wimbo wenyewe unahitaji mandhari ya nchi za kiarabu hata ukiangalia beat ipo kama kiarabu fulani hivi,” ameongeza.
Tunda Man amedai kuwa bajeti ya kukamilisha video hiyo ni zaidi ya shilingi milioni 14.
Katika hatua nyingine Tunda Man ameshare picha ambazo hajaeleza ni za nini japo zina dalili za kuwa ni video.
10990543_360654430789555_511366783_n
929224_536984433111216_246364816_n
10986304_786600978075411_1435630091_n
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment