Watu 10 wapoteza maisha baada ya helikopta mbili kugongana hewani wakati wakishoot reality show

Watu 10 wakiwemo wanamichezo wa olimpiki wa Ufaransa walioshindana kwenye mashindano hayo ya London 2012 wamekufa baada ya helikopta mbili kugongana hewani nchini Argentina jana. Watu hao walikuwa kwenye mchakato wa kutengeza kipindi cha TV.
267DE53900000578-2987375-image-m-9_1425974290208
Washindi wa Olimpiki Camille Muffat, katikati, Florence Arthaud, wa pili kutoka kulia na Alexis Vastine wa mwisho kulia wakiwa pamoja na washiriki wenzao wakiwa njia kwenda kushoot kipindi cha reality cha ‘Dropped’. Mchezaji wa zamani wa Arsenal, Sylvain Wiltord (katikatia kushoto) alikuwa kwenye show hiyo lakini hakuwa amependa kwenye helikopta hizo

Camille Muffat, 25, mwogeleaji aliyeshinda midani ya dhahabu kwenye shindano la wanawake la 400m freestyle mwaka 2012, bondia wa olimpiki, Alexis Vastine, 28, aliyeshinda midani ya fedha kwenye mashindano hayo yaliyofanyika Beijing, 2008 ni miongoni mwa waliopoteza maisha.
267B722D00000578-2987375-image-m-4_1425951018749
Waliopoteza maisha ni pamoja na marubani wawili wa Argentina na raia wengine watano wa Ufaransa waliokuwa wakishiriki kwenye kipindi kiitwacho Dropped.
Mamlaka zimesema hadi sasa haijulikani chanzo cha ajali hiyo iliyotokea magharibi mwa jimbo la La Rioja jirani la milima ya Andes.
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment