BAADA YA SHULE YA SEKONDARI YA IFUNDA KUFUNGWA KWA VURUGU UONGOZI WA SHULE HIYO WAWAITA WANAFUNZI 28

 Mkuu wa shule ya sekondari ya Ifunda akizungumza na wanafunzi hao hivi karibuni.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Ufundi Ifunda.
Uongozi wa shule ya sekondari ya Ufundi Ifunda  mkoani  Iringa  imewaita wanafunzi 28 kufika shuleni hapo octoba 2 ikiwa ni baada ya  shule  hiyo  kufungwa kwa muda  usiojulikana kutokana na  wanafunzi  hao kufanya  vurugu kubwa  hivi karibuni.
Hatua ya uongozi wa shule hiyo kuwaita wanafunzi hao imekuja zikiwa ni zaidi ya siku 4 kupita toka shule hiyo kufungwa kufuatia vurugu kubwa shuleni hapo na  kusababisha  hasara  kubwa ya mali  za  shule  hiyo.
Makamu mkuu wa shule hiyo  Ernest Sakafu ameyasema hayo Leo wakati akizungumza na mtandao wa matukio daima ofisini kwake.
Amewataja wanafunzi wanaotakuwa kufika shuleni hapo kuwa ni steven Nyiriri, petro Kalolo, Iddi Shaban, John Zephania, Edwin Rwegoshora, Adinan Mrisho Mtiti, Izengo Dotto, Gaspar Manyagi, Shemson Amoni ,Halid Omari, Said Sambo, Paschal lusukanija , Fred Kidava na Eliji Nguvila
 
Wengine ni Stambuli Daluweshi, Jackson Mlowe,Sidi Kayombo,Yusuph Makale , Joseph Antony ,Allan Laurent, Rose Kayombo, Enoce John, Rashid Kandoro, Abdul Zumo, Petro Silwimba, Joyce Nestory , Michael Kimario na Athuman Ahamad.
 
Alisema kuwa kwa sasa shule hiyo imefungwa kutokana na vurugu hizo hivyo shule hiyo itafunguliwa wakati wowote kuanzia sasa.
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment