Shilole bado ana nia ya kugombea ubunge kwenye jimbo lake la Igunga, lakini anahofia kuwa maisha yake yanaweza kuwa hatarini!
Shilole ameiambia Bongo5 kuwa amepokea simu nyingi kutoka Igunga
zinazomtaka ajitose kuwania nafasi hiyo, lakini bado yupo njia panda.
“Unajua siasa ni ngumu mimi bado nipo kwenye mjadala wa kugombea na
hii ni baada ya kuona watu wanataka kuongozwa, lakini bado nafikiria,”
amesema. “Nikiwa tayari nitagombea kupitia CCM. Kitu ambacho
kinaniogopesha kiukweli ukiangaliwa watu waliopita ni vijana tu wanakufa
mapema kutokana na mambo ya siasa. Siasa inahitaji moyo sana mimi ni
muoga sana, naogopa kufa watu wanauwana! Mtu unatamani lakini ndo
hivyo,” ameongeza.
“Mimi napigiwa simu nyumbani Igunga, watu wengi sana kila mmoja
ananiambia ‘tunakuhitaji ugombe yaani baada ya Rostam wananihitaji mimi!
Mimi bado nipo njia panda mpaka sasa hivi lakini muda ukifika kila kitu
mtasikia.”
Home / Bongo Movie /
Bongo yetu /
Ma Star wetu /
News
/ Shilole naye autamani ubunge mwaka huu 2015 alitolea macho jimbo la zamani la Rostam Aziz
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment