Shilole naye autamani ubunge mwaka huu 2015 alitolea macho jimbo la zamani la Rostam Aziz

Shilole bado ana nia ya kugombea ubunge kwenye jimbo lake la Igunga, lakini anahofia kuwa maisha yake yanaweza kuwa hatarini!
11111519_1423638237948977_1431528597_n
Shilole ameiambia Bongo5 kuwa amepokea simu nyingi kutoka Igunga zinazomtaka ajitose kuwania nafasi hiyo, lakini bado yupo njia panda.
“Unajua siasa ni ngumu mimi bado nipo kwenye mjadala wa kugombea na hii ni baada ya kuona watu wanataka kuongozwa, lakini bado nafikiria,” amesema. “Nikiwa tayari nitagombea kupitia CCM. Kitu ambacho kinaniogopesha kiukweli ukiangaliwa watu waliopita ni vijana tu wanakufa mapema kutokana na mambo ya siasa. Siasa inahitaji moyo sana mimi ni muoga sana, naogopa kufa watu wanauwana! Mtu unatamani lakini ndo hivyo,” ameongeza.
“Mimi napigiwa simu nyumbani Igunga, watu wengi sana kila mmoja ananiambia ‘tunakuhitaji ugombe yaani baada ya Rostam wananihitaji mimi! Mimi bado nipo njia panda mpaka sasa hivi lakini muda ukifika kila kitu mtasikia.”
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment