Muigizaji wa filamu ya ‘Chausiku’, Shamsa Ford amemmwagia sifa rapper
Nay wa Mitego kwa kudai hakuwahi kujua kama ni mkarimu huku akidai kuwa
anafaa kuwa mume!
Shamsa ambaye aliachana na mume wake tangu October mwaka jana,
ameiambia Bongo5 kuwa aliombwa na Nay ashirikishwe katika filamu yake.
“Sisi ni washkaji sema Nay ana kazi yake ya filamu ndio akaona mimi
ndo nafaa, Hakuna kitu chochote zaidi ya kazi,” amesema Shamsa.
“Kabla ya kupata nafasi ya kuongea na Nay nilikuwa namuona ni mtu fulani
mgomvi mgomvi, in short nilikuwa simpendagi! Kama unakumbuka aliwahi
kutuponda Bongo Movie na mimi kuna siku nilihojiwa na kituo kimoja
nikamponda sana! Lakini nimekuja kukutana na Nay nimegundua ni mtu
tofauti sana. Sasa hivi mimi namzungumzia Emmanuel is man ambaye kila
mtu au kila mwanamke anaweza akamhitaji kuwa naye! Ana huruma ana
upendo, he is a good man, kama nilivyosema mwanamke yoyote atapenda
kuwa naye. Kwahiyo ni husband material,” aliongeza Shamsa.
Kwa upande mwingine, Shamsa amewataka mashabiki wa kazi zake kutambua
kuwa yeye ni mtu mzima na ana maamuzi ya kufanya kile anachokipenda ili
mradi asiharibu kazi.
“Mashabiki wangu wajue Shamsa mimi najielewa najitambua ni mkubwa na
ninajua zuri na baya,” amesisitiza muigizaji huyo. “Wasinihukumu kwa
ambacho wanakiona au wanachokisikia, wanisubiri mimi kama mimi Shamsa na
hayo wanayoyasikia hayawezi kuniharibia mimi kazi zangu au kuachana
mimi na mume wangu ndo nitashuka kisanii, hapana! Wasihukumu hivyo, mimi
nipo makini na kazi zangu.”
Home / Bongo Movie /
Bongo yetu /
isikupite
/ Shamsa Ford: Nay wa Mitego ni mwanaume anaye faa kuitwa mume
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment