TAIFA STARS KUPIMANA UWEZO NA RWANDA LEO TAREHE 21/JAN/2015(CCM-KIRUMBA MWANZA)

 

LEO Taifa Stars Maboresho inacheza mechi ya kirafiki na Rwanda ya Haruna Niyonzima kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, lakini Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limefanyia marekebisho kanuni zake za michuano ya ngazi ya klabu kwa upande wa malazi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), CAF imesema kuanzia sasa timu zitachagua na kujilipia zenyewe hoteli zinapokuwa kwenye mechi za ugenini.

Kabla ya marekebisho ya kanuni hiyo, timu ngeni ilikuwa ikilipiwa hoteli na timu mwenyeji kwa msafara usiozidi watu 25. CAF ilikuwa imepitisha hoteli maalumu katika kila nchi ambapo mwenyeji alitakiwa kuziweka timu ngeni.

Kwa marekebisho hayo, chama cha soka cha nchi mwenyeji kitakuwa na wajibu wa kuitafutia hoteli timu ngeni iwapo tu kitaombwa kufanya hivyo, lakini jukumu la kulipia malazi litakuwa la timu yenyewe.
 
Mwaka huu Tanzania inawakilishwa na timu mbili za Azam na Yanga katika michuano ya CAF ambapo Azam itacheza Ligi ya Mabingwa na Yanga itacheza Kombe la Shirikisho Afrika. Yanga itacheza Februari 14, mwaka huu na BDF IX ya Botswana na Azam itacheza na El Merreikh ya Sudan Februari 15 kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam.

Wakati huohuo, Taifa Stars Maboresho inayoongozwa na Simon Msuva leo Alhamisi inacheza mechi ya kirafiki na Rwanda ‘Amavubi’ jijini Mwanza kwa lengo kuboresha kikosi hicho kwani mchezo huo hautambuliwi na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment