JAJA NI SHIDA SIMBA







USAJILI wa mafowadi uliofanywa na mahasimu wa Simba kwenye Ligi Kuu Bara, Yanga, umeitisha klabu hiyo na maofisa wake wameamua kupiga kambi jijini Kigali kwenye Kombe la Kagame mpaka impate beki wa maana.
Simba ambayo Mwenyekiti wake wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Poppe yupo mjini Kigali, tayari imempata na kumtanguliza Unguja, Zanzibar beki wa Telecom ya Djibout ambaye ni raia wa Burundi, Butoyi Hussein na jana Jumatano jioni alianza matizi na timu.
Kiongozi huyo alisema kwamba wanahitaji kufanya usajili wa beki imara wa kupambana na fowadi kama ya Yanga yenye straika, Mbrazil Genilson Santos ‘Jaja’, Emmanuel Okwi pamoja na Azam iliyosajili washambuliaji kutoka Ivory Coast, Haiti na Burundi.
Hans Poppe ameiambia Mwanaspoti jijini Kigali kwamba wameangalia ufanisi wa kikosi kwenye mechi ya Simba Day dhidi ya Zesco wakagundua kwamba wanahitaji kufanya mabadiliko haraka.
Mbali na hilo pia kigogo huyo mwenye ushawishi mkubwa Msimbazi, alisema wanataka kutafuta beki imara ili wampe mkono wa kwaheri, Donald Mosoti ambaye amewaambia wamuache aende Qatar.
“Mosoti anataka kwenda Qatar ndio maana tunatafuta beki wa maana kwenye haya mashindano, tukifanikiwa tu tunamuacha Mosoti aende zake. Yule Butoyi tumemtanguliza kwamba kocha amuangalie mazoezini, akikubaliana naye sawa tutamsainisha rasmi,” alisema.
“Lakini vinginevyo inabidi tuendelee kutafuta mwingine tena. Tunataka kuwa na beki katili na mbishi asiyekubali matokeo kirahisi, ukiangalia wapinzani wetu wameisuka upya safi yao ya ushambuliaji hatutaki kuwaangalia wao sana, lakini tunataka kuwa tayari na aina yoyote ya washambuliaji wasumbufu.”
Mosoti aliiambia Mwanaspoti jana kwamba yupo tayari kuondoka dakika yoyote kama uongozi ukimruhusu.

 
PHIRI ATAKA VIDEO
ZA MOSOTI
Kocha Patrick Phiri, ameuagiza uongozi wa Simba kumpelekea video za mechi ya Nani Mtani Jembe na nyingine mbili walizocheza na Yanga msimu uliopita ili kuangalia kiwango cha wachezaji wake wawili, beki Mkenya Donald Mosoti na kiungo Jonas Mkude ambaye kwa sasa ni majeruhi.
Awali, Mosoti aliomba kuvunja mkataba wa timu hiyo ili aende kucheza katika moja ya timu alizopata Qatar, hivyo huenda ujio wa Hussein ukamfanya Mosoti kuondoka ambapo yeye amekiri kuwa atakuwa tayari kuondoka muda wowote.
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment