Kombe la AFCON 2017 kuchezwa nchini Gabon

Shirikisho la soka barani Afrika CAF limetaIngaza Gabon kuwa itakuwa mwenyeji wa mashindano ya kombe la mataifa ya Afrika ya mwaka 2017.
caf_logo
Rais wa shirikisho hilo, Issa Hayatou alitangaza kutoka Cairo, Misri
Libya ndio nchi iliyokuwa iandae michuano hiyo lakini iliomba iondolewe kwenye nafasi hiyo kutokana na hali ya usalama kuwa sio nzuri.
CAF limeichagua Gabon iliyokuwa ikigombea nafasi hiyo pamoja na Ghana na Algeria ambayo huenda imepoteza nafasi hiyo kutokana na hali ya usalama katika viwanja vyake baada ya tukio la kifo cha mchezaji wa Cameroon, Albert Ebosse mwaka 2014.
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment