Pamoja na kufariki kwa muigizaji wake muhimu Paul Walker mwaka juzi,
filamu ya Fast & Furious 7 inatarajiwa kuingiza makadirio ya faida
ifikayo dola bilioni 1.37.
“Furious 7” inaweza kuingiza dola milioni 119 za mauzo ya tiketi
katika weekend yake ya kwanza na dola milioni 283 kwenye majumba ya
sinema nchini Marekani na Canada kwa mujibu wa BoxOffice.com.
Hiyo itafanya “Fast & Furious” kuwa filamu ya mfululizo hiyo
yenye mafanikio zaidi kuliko zote. Kwa pamoja filamu za kwanza sita
ziliingiza dola bilioni 2.38.
Walker alifariki akiwa na umri wa miaka 40 kwa ajali mbaya ya gari November 2013.
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment