Moja ya mjadala ambao umechukua nafasi
kubwa leo mitandaoni ni kuhusu ishu ya uamuzi uliotolewa na Mahakama Kuu
kuhusu kesi iliyofugiliwa na Mbunge Zitto Kabwe.
Taarifa iliyoenea mitandaoni na
kuripotiwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari inasema Mahakama
imetupilia mbali kesi ambayo ilifunguliwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini,
Zitto Kabwe kuhusu kujadiliwa uanachama wake ndani ya chama hicho, ambapo katika hukumu hiyo Zitto ametakiwa pia kulipa gharama zote za kuendesha kesi hiyo.
Zitto Kabwe amepata nafasi ya kuongelea hilo>>‘Mimi nilikuwa kwenye kikao cha Mamlaka ya EWURA nikajulishwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa kesi yetu imetupwa’
‘Lakini
kwenye kumbukumbu zetu ilikuwa twende Mahakamani tarehe 12 mwezi wa 3
sio kwa ajili ya maamuzi ni kwa ajili ya kesi kutajwa, kwetu sisi
tumeshangazwa kwamba kesi imefanyika leo kwa maamuzi kesi ambayo
ilipaswa itajwe vile vile siku hiyo hiyo Chadema kutangaza kwamba
wamenivua uanachama mimi mpaka sasa sina taarifa rasmi na naendelea na
kazi zangu kama kawaida’
Kwenye sentensi nyingine Zitto Kabwe amesema;
‘leo nilikua na EWURA.. ratiba yangu inaonyesha kesho nitakuwa na
TANESCo na keshokutwa nitakuwa nashughulikia mabilioni ya Uswisi’
‘Kwa
upande wangu mimi taarifa yoyote rasmi sina, nitaweza kusema chochote
baada ya kupata taarifa rasmi.. Wanasheria wangu wamekwenda Mahakamani
kwa ajili ya kupata hiyo Judgement na kuweza kuona hatua gani
zitakazofuata katika hiyo Judgement’– Zitto Kabwe.
Bonyeza play kumsikiliza Zitto Kabwe.
0 comments:
Post a Comment