MASHINE YA KUPULIA YA BOBBY BROWN ITAZIMWA KESHO SIKU SAWA NA ILE ALO FARIKI MAMA YAKE


Bobbi Kristina akiwa na mama yake mzazi, Whitney Houston enzi za uhai wake.
FAMILIA za Bobby Brown na marehemu Whitney Houston zimekubaliana kumwondolea Bobbi Kristina mashine inayomsaidia kupumua kesho, Jumatano ili afe tarehe sawa na ile ambayo mama yake mzazi, Whitney Houston alifariki.
Bobbi Kristina Brown.
Mjukuu wa Bobbi, Cissy Houston alitoa wazo hilo la Februari 11 wakati wa majadiliano yaliyofanyika wikiendi iliyopita kati ya familia ya Whitney Houston na Bobby Brown kwenye Hospitali ya Chuo Kikuu cha Emory huko Atlanta nchini Marekani.
Bobbi Kristina Brown akiwa na mpenzi wake Nick Gordon.
Brown alitoa baraka zake kuruhusu binti yake huyo aondolewe mashine ya kupumua wakati wa usiku ili afe tarehe moja ya Februari 11 sawa na mama yake aliyefariki Februari 11, 2012 katika Hoteli ya Beverly Hilton.
Maamuzi hayo yamefikiwa ili kuweka kumbukumbu ya mama na binti yake ili wote wapumzike kwa amani, familia ya Brown ilieleza.
Bobbi Kristina, 21, binti pekee wa Houston na mwimbaji Bobby Brown, amepoteza fahamu tangu alipokutwa bafuni hakiwa hajitambui Januari 31, mwaka huu.
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment