Waandaaji wa Tamasha la Kiswahili
Washington DC Ndugu Patrick Kajale na Dada Finiana wakijadili jambo na
ndugu Safari ambaye ndiye Mtunzi wa kile kitabu Nambari moja Amazon cha
Nyayo za Obama.
Nyama Choma katika banda la Safari Restaurant Washington DC,Safari ni Mgahawa wa Kitanzania uliopo katika jiji la Washington ambapo vyakula vingi vya kinyumbani vinapatikana.
Ice Cream au lamba lamba kama zinavyojulikana kwa kiswahili pia zilikuwepo kwa ajili ya watoto na watu wazima
Miss Temeke- CEO wa Kwetu Fashion Design akiwa katika Meza yake baada ya kumaliza Maonyesho yake ya Mavazi ya Kitanzania.
Nguo za kina Kaka kutoka kwetu fashion Design By Miss Temeke Patrick Kajale nae akipita katika Vazi la Kimasai
Kwa Upande wa burudani
walikuwepo pia Wasanii Mahiri wa kizazi Kipya Wakitanzania na East
Afrika kwa ujumla waishio Marekani kama AJ Ubao,Prince Herry,Max na
Jumbe Mr TZ Mwanadada "Senai" Mpiga Gitaa Maarufu kutoka Afrika Mashariki anayeishi Marekani
Mikono Juu..Prince Herry akiwarusha Watazamaji kwa Ufasaha na Style yake ya lay back.Prince Herry Akifokafoka kwa hisia kali katika kile kibao chake kinachoitwa "Au Sio"
Kijana Max Ambaye watu wengi wanamwita Silent Killer aliwarusha watazamaji vilivyoJumbe Mr Tanzania aliwarusha watazamaji kwa style yake yakipekee huku Mwanamuziki AJ Ubao akimsindikiza kwa nyuma
Kwa mara
ya Kwanza kabisa nchini marekani limefanyka tamasha la Kiswahili katika
jiji la Washington, likijumuisha nchi zote za Afrika Mashariki na kati
zinazozungumza lugha ya kiswahili.Tamasha hili liliandaliwa ili kuweza
kutangaza tamaduni za Afrika Mashariki ikiwa ni pamoja na Chakula,
Mavazi, Ngoma za Asili, Miziki ya Kizazi Kipya,na mambo mbali mbali ya
kiasilia.
Waandaaji
Wanatoa Shukrani Kwa watu wote waliojitokeza kwani hii ni mara ya
kwanza kabisa Tamasha kama hili kufanyika nchini Marekani hivyo
tutegemee Mambo mengi Makubwa Mwakani kwani Huu ni Mwanzo.
0 comments:
Post a Comment