Simba yaiwahi Yanga Zanzibar

Simba ilimalizana na Kiongera lakini ilimruhusu kurudi kwao kuisadia timu yake ya KCB katika mechi za Ligi Kuu Kenya (KPL) ili iepukane na hatari ya kushuka daraja kutokana na kupata matokeo mabaya kwenye mechi zake za awali.
SIMBA jana Ijumaa iliondoka kwenda Unguja, Zanzibar kuweka kambi yake kwa ajili ya maandalizi ya Ligi Kuu Bara huku ikimwacha mshambuliaji wake Mkenya, Paul Kiongera aliyepo Nairobi na anatarajia kujiunga na timu hiyo wiki ijayo. Yanga nayo itatua Zanzibar Jumatatu.
Simba ilimalizana na Kiongera lakini ilimruhusu kurudi kwao kuisadia timu yake ya KCB katika mechi za Ligi Kuu Kenya (KPL) ili iepukane na hatari ya kushuka daraja kutokana na kupata matokeo mabaya kwenye mechi zake za awali.
Kwa sasa Simba ipo chini ya kocha mpya Mzambia Patrick Phiri ambaye alianza kazi ya kuifundisha mara baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja juzi Alhamisi. Simba iliondoka jana saa 10 jioni kwa boti ya Azam Sea Express.
Akizungumza na Mwanaspoti, Rais wa Simba, Evans Aveva, alisema timu itakaa huko mpaka ligi itakapoanza ingawa alidai kuwa endapo kutakuwapo na mechi za kirafiki watakuja jijini kucheza na kurudi Zanzibar.
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment