MASHIRIKISHO YA SANAA NCHINI YATUA BUNGE LA KATIBA KUFUKUZIA HOJA ZAO

pix 1Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mh. Samuel Sitta (kulia), akisisitiza jambo kwa wawakilishi wa mashirikisho ya sanaa mjini Dodoma hivi karibuni. Mashirikisho hayo yamekuwa yakipambana kufa na kupona kuhakikisha katiba mpya inatambue wasanii kama kundi maalum na pia ilinde mali zisizoshikika yaani miliki bunifu (intellectual property). Maoni ya mashirikisho hayo yalishatolewa katika hatua za awali za utoaji maoni na pia kupitia mabaraza lakini kwa bahati mbaya, hayakujumuishwa katika rasimu. Waliokaa kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki Tanzania, Bw. John Kitime, Rais wa Shirikisho la Filamu, Bw. Simon Mwakifwamba na Makamu mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Bi. Samia Suluhu Hassan. (Picha zote kwa hisani ya ofisi ya Bunge la Katiba).
pix 3Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mh. Samuel Sitta akikabidhiwa nyaraka yenye hoja ya uzengezi (lobbying) kutoka kwa kiongozi wa msafara wa mashirikisho ya sanaa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Bw. Simon Mwakifamba, mjini Dodoma hivi karibuni. pix 5Makamu Mwenyekiti  wa Kamati namba tano ya Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Assumpter Mshama, akishibishwa hoja za kina kwa nini wasanii wanataka katiba mpya itambue wasanii kuwa kundi maalum na pia ilinde mali isiyoshikika au kwa lugha nyepesi miliki bunifu (intellectual property) toka kwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki Tanzania, Bw. John Kitime, mjini Dodoma hivi karibuni.
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment