MTANGAZAJI wa Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty’, juzikati alijikuta akitwangana makonde na mrembo mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja baada ya kupishana kauli kwenye ukumbi mmoja wa starehe pande za Kahama, Shinyanga.
Mtangazaji wa Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty
Katika tukio hilo, Fetty aliyekuwa kwenye ‘tour’ ya Serengeti Fiesta alizama ukumbini hapo usiku na baada ya muda mfupi paparazi wetu alishangaa kumuona akizichapa na mrembo huyo ikidaiwa walizinguana, hata hivyo waliamuliwa kabla mambo hayajawa mabayaw.
Ziara ya Tamasha la Fiesta kesho itahamia Tanga ambapo wasanii kibao wataangusha burudani ndani ya Uwanja wa Mkwakwani.
Share on Google Plus

About ahmed

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment